FAMILIA YA REEVA STEENKAMP YAPINGA UAMUZI WA JAJI..............

Familia ya Reeva Steenkamp
ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi na mwanariadha wa Afrika kusini Oscar Pistorius imekasirishwa na uamuzi wa jaji wa kesi hiyo baada ya kumpata na hatia ya mauaji ya kutokusudia na kumuondoalea mashtaka ya mauaji.
June Steenkamp amesema kuwa mwanawe ambaye alikufa vibaya hakufanyiwa haki.
Amesema kuwa hakuamini kwamba jaji wa kesi hiyo alikubali ushahidi wa Oscar Pistorius kwamba alidhani bi Reeva Steenkamp alikuwa mtu ambaye alikuwa amevamia nyumba yao.
Hatahivyo mjombaake Pistorius alimshukuru jaji huyo kwa kumuondolea mashtaka ya mauaji mwanariadha huyo.
Oscar Pistorius ataendelea kuwa nje kwa dhamana hadi hukumu yake itakapotolewa mnamo mwezi ujao.

Popular posts from this blog