USIYOYAJUA KUHUSU UAMISHO WA WELBECK........KUMBE MANCHESTER ILIMPA PESA ILIAONDOKE.......
BEKI wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand ameponda na
kuhoji uamuzi wa timu hiyo kumpiga bei Danny Welbeck
hasa kwa wapinzani wao Arsenal.
hasa kwa wapinzani wao Arsenal.
Wakati Rio akishindwa kupata majibu, imefichuka
kwamba United chini ya kocha wake mpya, Louis van Gaal, ilimlipa pesa
Welbeck ili kukamilisha uhamisho wake wa kwenda Arsenal uliogharimu
Pauni 16 milioni.
Welbeck, ambaye ametokea kwenye akademia ya klabu
hiyo ya Old Trafford alipogundua analazimishwa kuhama aliomba alipwe
pesa kitu ambacho United ilikifanya na kumlipa Pauni 1.5 milioni ili
aende Arsenal.
Welbeck aliwekwa kwenye orodha ya wachezaji ambao hawakuwa kwenye mipango ya kocha Van Gaal kwenye klabu hiyo ya Old Trafford.
Hatimaye, straika huyo Mwingereza amekwenda
kujiunga na Arsenal na kukabidhiwa jezi yenye Namba 23 atakayovaa na
miamba hiyo ya Emirates.