EBOLA YAZIDI LETA TISHIO NIGERIA...........
Shirikisho la walimu nchini humo linaitaka serikali kuchukua hatua ili kuzuia tishio la maambukizi ya ugonjwa wa ebola kwa wanafunzi, na kusema kuwa wamesitisha mgomo
Wakati huo huo, Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa maambukizi ya virusi vya ebola yamedhibitiwa nchini Nigeria na Senegal miongoni mwa nchi tano ambazo ugonjwa wa ebola umeua karibia watu 2800.
Raia wa Nchi jirani Sierra Leone walilazimika kujifungia ndani wa mda wa siku tatu kujinusuru na ebola zoezi ambalo viongozi wamesema kuwa limefanikiwa.