TALAKA YA AMBER ROSE NA WIZ KHALIFA: Kila mmoja anamshutumu mwenzie kuchepuka


Ndoa ya Wiz Khalifa na Amber Rose imefika ukingoni
 Amber Rose anamshutumu Wiz Khalifa kuwa
 amekuwa akimsaliti kwa kipindi kirefu na kumtolea sababu 
zisizo na kichwa wala wa miguu

Vyanzo vilivyo karibu na Amber vimeiambia TMZ kuwa tangu kuanza kwa ziara ya Wiz
 July mrembo huyo amekuwa akimhisi mume wake kuchepuka. Amber anawaambia 
marafiki zake kuwa  
alitaka kuungana na Wiz kwenye ziara hiyo lakini (Wiz) alikataa na
 kumtaka akae nyumbani 
kumwangalia mtoto wao
Anadai kuwa Wiz anataka kumtawala zaidi kwa kusema yeye ndiye
 anatakiwa kutafuta mkate wa 
kila siku na Amber akae tu nyumbani
Naye Wiz anadai kuwa ni Amber ndiye aliyemsaliti na Nick Cannon

     
Kupitia talaka hiyo, Amber anataka kuchukua udhibiti wa mtoto 
wao Sebastian,mwenye umri
wa mwaka mmoja lakini atamruhusu Wiz kumtembelea mwanae.TMZ imedai
 imeziona nyaraka 
za talakaambazo 
zinaonesha 
kuwa wapenzi hao waliachana Jumatatu hii kwa kile kilichodaiwa tofauti 
zisizosuluhishika

Popular posts from this blog