JENEZA LAKUTWA NDANI YA NYUMBA YA MTENDAJI WA KIJIJI............

jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linawasaka watu wasiofahamika wanaotuhumiwa 
kuingia msikitini na kuiba jeneza, Wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma.Baada ya
 kuiba jeneza hilo, watu hao wanadaiwa 
kwenda nyumbani kwa Afisa wa Kijiji cha Kitanda, wilayani humo, Fidea Mbawala
na 
kuliweka mlangoni, likiwa limesheheni matofali
Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Mihayo Msikhela, alisema tukio hilo lililotokea juzi,
 saa 12:00 asubuhi, katika kijiji hicho  
Alisema tukio hilo limesababisha kuwapo utata na kwamba uongozi wa 
msikiti umedai kuwa tukio hilo ni la aina yake, ambalo halijawahi kutokea 
Alisema tukio hilo liligundulika wakati waumini wa msikiti huo 
walipokwenda kuswali swala ya alfajiri na kushtuka baada ya kusikia kuwa
 jeneza hilo limekutwa kwenye mlango wa nyumba ya afisa mtendaji wa 
kijiji hicho
Alisema kwa mujibu wa Katibu wa Msikiti huo, Khalifa Ngonyani, tukio hilo limezua
 mtafaruku mkubwa kwa waumini wa msikiti huo  
Kamanda Msikhela alisema taarifa za awali zinaonyesha kuwa tukio hilo  
limefanyika baada ya afisa huyo kuwaeleza wananchi wa kijiji chicho kuwa
 wanatakiwa kuchangia asilimia 75 ya ujenzi wa shule ya kutwa ya 
sekondari ya Mkomanile
Alisema ujenzi wa shule hiyo ni utekelezaji wa agizo lililotolewa na   
Rais Jakaya Kikwete na kwamba, wanakijiji waligoma kutoa michango hiyo 
kwa madai kwamba, agizo hilo ni la ghafla na kuomba wachangie mwaka 
2015, kwani kwa sasa nguvu zao wameelekeza kwenye kilimo
Msikhela alisema hakuna mtu aliyekamatwa na kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi 

Popular posts from this blog